STARS YAANZA VIBAYA AFCON,YATANDIKWA 3-0 NA MOROCCO

TAIFA Stars  imeanza vibaya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya kutandikwa mabao 3-0 na Morocco katika mchezo wa Kundi F uliopigwa  usiku huu Uwanja wa Uwanja wa Laurent Pokou Jijini San-Pedro, Ivory Coast. 

Katika mechi hiyo Stars  ilimaliza pungufu baada ya kiungo wa  Novatus Dismas Miroshi kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 70 kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.

Morocco ilijipatia mabao yake kupitia na beki  Romain Ghanem Paul Saïss , kiungo  Marseille  Azzedine Ounahi na mshambuliaji na Youssef En-Nesyri.

Comments