KIPA MZUNGU ATUA YANGA KWA MAJARIBIO, WAGHANA NAO RASMI


IVAN KNEZEVIC AKISHUKA KATIKA GARI LA YANGA MARA BAADA YA KUWASILI KATIKA JENGO LA KLABU HIYO AMBAPO YEYE NA WACHEZAJI WENGINE KUTOKA GHANA WAMEWASILI LEO ASUBUHI.

KIPA kutoka Serbia Ivan Knezevic amewasili nchini tayari kwa majaribio  katika klabu ya Yanga na iwapo atafanikiwa katika hilo atasajiliwa kuichezea timu hiyo kwenye msimu ujao wa Ligi Kuuu Bara utakaoanza Augusti 21 pamoja na michezo mingine ya kimataifa.



Mbali na Kipa huyo, pia wachezaji wanne kutoka Ghana nao wamewasili tayari kuichezea klabu hiyo.

Wachezaji hao ni pamoja na Isack Boakye (Mlinzi wa Kati), Keneth Asamoah (Mshambuliaji wa Kati),
Ernest Boakye (Kiungo) pamoja na Yaw Berko ( Kipa) ambaye alikuwemo katika msimu uliopita.

Comments