MWAKINYO ACHAGIZA MAPRO

 BONDIA Hassan Mwakinyo amesema mapromota wanaotaka kumewekea gari kwa ajili ya pambano milango iko wazi.

Mwakinyo aliandika ujumbe huo jana kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii akisema sasa yuko tayari kwa mapromota wanaotaka kumewekea gari kwa ajili ya kupigana kama zawadi.

“Haya sasa mapromota anayetaka kuniwekea gari milango iko wazi,”ulisomeka ujumbe huo huku akiwa ameweka picha ya gari kuonesha umuhimu wake.

Haitakuwa mara ya kwanza hapa nchini kwa bondia kupigana kwa ushindi wa gari kwani bondia kutoka Morogoro Twaha Kassim ‘Kiduku’ aliwahi kupigana na kushinda gari aina ya Toyota Crown mwaka juzi.

Mwakinyo kwa sasa anajiandaa na pambano la usiku wa Mtata Mtatuzi litakalopigwa Januari 27 mwaka huu kwenye Uwanja wa New Amaan Zanzibar dhidi ya bondia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mbiya Kanku kuwania mkanda wa dunia wa WBO.

Comments