MEXIME AWAPIGA MKWARA WACHEZAJI WAKE

 Kocha Mkuu wa Ihefu FC, Mecky Maxime  amewataka wachezaji wake kutumia vipaji vyao ipasavyo ili kuipa matokeo mazuri timu hiyo.

Maxime alisema nafasi waliyopo kwenye msimamo haiendani na ukubwa wa majina na umaarufu waliokuwa nao wachezaji wake

“Ligi ya msimu huu ni ngumu inahitaji wachezaji wanaopambana na siyo umaarufu au ukubwa wa majina mimi na vijana wangu tunapaswa kupambana na kila mmoja kutimiza wajibu wake   ili kuiondoa timu kwenye nafasi mbaya iliyopo hivi sasa,” alisema Maxime.

Aliongeza kuwa  usajili walioufanya kwenye dirisha dogo ni mzuri na unakwenda kuwaongezea nguvu lakini kitu cha kwanza lazima kila mtu atimize jukumu lake la msingi.

Aliongeza kuwa na wachezaji wazuri wazuri siyo kitu muhimu sana kama wachezaji hao hawajitumi hivyo atahakikisha anaanda mpango mkakati maalumu utakaomwezesha kila mchezaji kuchangia mafanikio waliyoyakusudia.

Ihefu iliyopo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu   imefanya usajili mkubwa kwenye dirisha dogo baadhi ya wachezaji iliyo wasajili ni Elvis Rupia, Duke Abuya na Bruno Gomes wote kutoka Singida Fountain Gate 

Comments