LOMALISA 'AJIFUNGA' MMOJA TENA YANGA

 BEKI wa kushoto wa Yanga, Joyce Lomalisa ameongeza mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kuitumikia timu hiyo.

Mkataba wa awali wa beki huyo unamalizika mwishoni mwa msimu huu hivyo uongozi kwa kushirikiana na benchi la ufundi umeamua kumuongeza mwaka mmoja kutoka na kuvutiwa na huduma yake.

Lomalisa alisema kilichomfanya kukubali kuongeza mkataba mpya ni malengo waliyokuwa nayo viongozi wa timu hiyo hasa katika mashindano ya kimataifa.


“Yanga ni sehemu salama kwangu viongozi wake wana maono ya mbali ndiomaana nimechagua kubaki hapa naamini nitafika mbali zaidi hasa katika mashindano ya kimataifa,” alisema Lomalisa.

Beki huyo alisema katika kipindi cha misimu miwili ambacho ameichezea timu hiyo amebaini mambo mengu mazuri ikiwemo kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kufika fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu uliopita na kubeba ubingwa wa Ligi Kuu na Kombe la FA.

Alisema kwa sasa akili na mawazo yake ameyaweka kwenye klabu hiyo kuhakikisha anashirikiana na wenzake ili kuipa mafanikio zaidi katika mashindano yote ambayo wanashiriki msimu huu.

Lomalisa alijiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili mwanzoni mwa msimu huu akitokea Petro Atletico ya Angola na tangu ajiunge amekuwa na mchango mkubwa kwenye kikosi cha kocha

Comments