MABINGWA wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Yanga leo wametoka
sare ya bao 1-1 na mabingwa wa Uganda, Kampala City Councel (KCC) katika mchezo
uliopigwa kwenye dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa ni wa kirafiki, Yanga
ilianza kutikisa nyavu za KCC kupitia kwa kiungo wake mpya, Hamis Sadick kabla
ya Kavu Mawini kusawazisha dakika chache
baadaye.
Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi Ernie Brandts ameshukuru
viwango vilivyooneshwa na wachezaji wake na hasa ikizingatiwa kuwa walicheza na mabingwa
wenzao.
Brandts alisema ameona viwango walivyonavyo wachezaji wake
hivyo atafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza.
Timu hizo zitarudiana kesho mjini Shinyanga katiika mchezo
utakaopigwa katika Uwanja wa kambarage mjini humo, kabka ya kuelekea mjini
Bukoba kucheza na timu watakayopangiwa na wenyeji wao.
Comments
Post a Comment