HATIMAYE kozi ya awali ya ukocha aliyoipata nahodha wa
zamani wa Yanga na timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, Shadrack Nsajigwa ‘Fusso’
imezaa matunda baada ya kupata kazi ya kuifundisha klabu ya Lipuli ya mjini
Iringa inayoshiriki Ligi daraja la kwanza.
Nsajigwa aklikuwa ni mmoja ya wahitimu wa kozi hiyo
iliyoandaliwa na chama cha soka mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kumalizika wiki
iliyopita.
Mwenyekiti wa Lipuli Abuu Changawa amesema kwamba wamemchukua Fusso kutokana na uzoefu wa
kucheza muda mrefu katika klabu ya Yanga pia ni mmoja ya wachezaji wenye
nidhamu hivyo atasaidia kuwaweka wachezaji katika nidhamu nzuri.
Alisema wamedhamiria kuhakikisha timu yao inautoa
kimasomasoa mkjoa wa Iringa ambao kwa zaidi ya miaka 10 umeshindwa kutoa timu
katika Ligi Kuu Soka Tanzania Bara.
Comments
Post a Comment