Wanamuziki hao watatu na wakongwe nchini ndio wanaounda kundi hilo litakalojulikana kwa jina la NDEGE 3
KUNDI jipya la muziki lijulikanalo kama
Ndege 3 limeanzishwa rasmi huku likiundwa
na wanadada wakongwe katika Tasnia ya
muziki wa dansi na kizazi kipya Joan matovolwa, Khadija Mnoga (Kimobitel) na
Paulyne Zongo.
Tayari kundi hilo
hivi karibuni limeshatoa kibao chake
kinachokwenda kwa jina la 'MISUKOSUKO YA MAPENZI' ambacho tayari kimeanza
kurushwa katika vituo mbalimbali vya redio nchini.
Joan Matovolwa na
Paulyne Zongo ni wanamuziki huru wakati Khadija Mnoga (Kimobitel) ni mwanamuziki
anayeimba katika bendi ya Extra Bongo inayoongozwa na Camarade Ally Choki.
Comments
Post a Comment