Tanzania Breweries Limited (TBL) chini ya nembo yake ya Kilimanjaro
Premium Lager, inaendelea na ‘Kili Music Tour 2013’ wikiendi
hii mjini Moshi.
Tamasha hili kubwa litafanyika Jumamosi ya tarehe 06 Julai, 2013, mjini Moshi kwenye kiwanja cha Ushirika na litajumuisha
wasaniii 10 ambao ni Barnaba,Diamond, AT, Snura Mushi, Professor J, Lady Jay
Dee, Roma, Kala Jeremiah, Joh Makini na Ben Pol.
“Tunashukuru kuwa
watanzania wamepokea tamasha hili kwa vizuri kabisa na wameshiriki kikamilifu
kwenye mikoa ya Dodoma na Tanga, hivyo basi tunategemea Moshi itajumuika nasi
ipasavyo kufanikisha tamasha litakalofanyika mkoani hapo Jumamosi ya tarehe 06.”
Alisema bwana George Kavishe meneja wa bia ya Kilimanjaro.
Bwana
Kavishe aliendelea kufafanua kuwa “bia ya Kilimanjaro Premium Lager inaendelea
kutoa bonge la kiburudisho kwa watanzania kwa kuhakikisha kuwa kila mkoa
unapelekewa wasanii mahiri kabisa wa muziki wa bongo fleva wawaburudishe
“kikwetukwetu”
Msanii wa muziki nchini Tanzania Diamond alinukuliwa
akisema kuwa “ kama kawaida yangu nimejiandaa ipasavyo kuhakikisha kuwa
ninawaburudisha mashabiki wangu ipasavyo. Hivyo basi msikose kuhudhuria na
kujionea ufanisi mahiri wa Diamond Platnumz.”Matamasha ya Kili Music Tour 2013 yatapumzika kwa muda wa mwezi mmoja na kurejea tena kuanzia tarehe 17 Agosti, 2013 kwenye mikoa mitano iliyobaki.
Comments
Post a Comment