Jumla ya makocha wa mpira wa miguu na walimu 28 kutoka
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na shule za msingi na sekondari
wameteuliwa kuhudhuria kozi ya FIFA 11 For Health inayoanza keshokutwa (Julai 7
mwaka huu) Homboro mkoani Dodoma.
Kozi hiyo itakayomalizika Julai 20 mwaka huu itakuwa chini
ya ukufunzi wa Rogasian Kaijage ambaye pia ni Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya
wanawake (Twiga Stars).
Washiriki ni Abdul Mikoroti (Shule ya Msingi Nzasa),
Baltazar Kagimbo (Shule ya Msingi Tabata Jica), Baraka Baltazar (Shule ya
Msingi Muhimbili), David Kivinge (Shule ya Msingi Temeke), Dismas Haonga
(Tambaza Sekondari), Exuperus Kisaka (Shule ya Msingi Mavurunza) na Hadija
Kambi (Shule ya Msingi Karume).
Hamis Chimgege (Shule ya Msingi Tusiime), Hobokela Kajigili
(Shule ya Msingi Buguruni), Issack Mhanza (Shule ya Msingi Airwing), Job
Ndugusa (Shule ya Msingi Upanga), John Sebabili (TFF), Lutta Rucharaba (Shule
ya Msingi Montfort), Maua Rahidi (Shule ya Msingi Uhuru Wasichana), Michael
Bundala (TFF) na Mussa Kapama (Shule ya Msingi Bunju ‘A’).
Priscus Silayo (Shule ya Msingi J.K. Nyerere), Peter Manyika
(TFF), Rajabu Asserd (Shule ya Msingi Mtoni Kijichi), Raphael Matola (TFF),
Raymond Rupia (St. Anne Maria Academy), Renatus Magolanga (Ulongoni Sekondari),
Ruth Mahenge (Shule ya Msingi Chang’ombe), Said Pambaleo (TFF), Sebastian Nkoma
(TFF), Titus Michael (TFF), Wane Mkisi (Jangwani Sekondari),
LIUNDA KUSIMAMIA
MECHI YA CHAN
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua Leslie
Liunda wa Tanzania kuwa Kamishna wa mechi kati ya Burundi na Sudan
itakayochezwa jijini Bujumbura.
Mechi hiyo ya kwanza ya mchujo ya Fainali za Afrika kwa
Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) itafanyika keshokutwa (Julai 7 mwaka huu).
Liunda anatarajia kuondoka leo usiku (Julai 5 mwaka huu) kwenda Bujumbura..
Comments
Post a Comment