SHIRIKISHO la Soka Tanzania
(TFF) limesema linafanyia kazi hoja ya klabu za Yanga na Simba kutaka kujitoa
kwenye michunao ya Kombe la Kagame zikihofia usalama wa Sudan Kusini.
Akizunguza kwa njia ya
simu jana jioni, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema baada
ya kuibuka hofu hiyo,
wanafanyia kazi jambo
hilo kabla ya kutoa tamko
rasmi.
“Tunalifahamu vizuri jambo
hilo. Tutakaa na kujadili kwa kina kabla ya kutoa tamko rasmi,” alisema
Angetile.
Kauli ya Angetile imekuja
siku moja tangu Simba na Yanga zitamke kujitoa kwenye michuano hiyo kama
itafanyika Darfur zikhofia hali ya usalama.
Juzi, kwa nyakati tofauti
viongozi wa Simba na Yanga, walisema wao wametafakari kwa kina tahadhari ya
Serikali kupitia kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Bernard Membe, hivyo hawakwenda Darfur.
Viongozi hao walitamka
wazi kuliacha jambo hilo mikononi mwa TFF kuamua nini kifanyike baada ya
tahadhari ya serikali kuona nini kifanyike.
Kwa upande wa Katibu Mkuu wa
Yanga Lawrance Mwalusako, aliisihi TFF kufuatilia halia halisi ya usalama
iliyopo Darfur.
Alisema pamoja na utayari wao
kucheza michuano hiyo, TFF inao wajibu wa kufuatilia mwenendo mzima kuhusu hali
ya usalama.
“Klabu tupo chini ya TFF, hivyo
hatuwezi kuamua kujitoa bila ya kupata baraka kutoka kwao. Ni wajibu wao
kufuatilia hali halisi kwanza na kutoa tamko juu ya ushiriki wetu,” alisema
Mwalusako, juzi.
Naye Kaimu Makamu Mwenyekiti
wa Simba, Joseph Itang’are ‘Kinesim’
alisema pamoja na hali tete ya Darfur, bado wanasikilizia uamuzi wa mwisho wa
TFF.
Alisema wakiwa washiriki,
wanaendelea na maandalizi ya michuano hiyo hadi pale itakapojulikana
mustakabali mzima wa michuano hiyo.
“Tunaisihi TFF kulitilia
maanani jambo hili
na kutoa tamko kwamba hatuwezi
kujiamualia tu wakati kuna chombo cha juu yetu,” alisema.
Michuano hiyo itakayoanza
Juni 18 hadi Julai 2, itajumuisha timu tatu za Tanzania ikiwemo Super Falcon ya
Zanzibar.
Wakati mara ya mwisha kwa
Simba kutwaa taji hilo ni mwaka 2002, Yanga ndio bingwa mtetezi wa michuanbo
hiyo baada ya kutetea taji hilo Julai 28, mwaka jana.
Timu nyingine ni Ports
(Djibout), Express (Uganda), Tusker
(Kenya), Al Merreikh, El Hilary na El Ahly Shandy (Sudan), APR (Rwanda),
Elman (Somalia), Vitalo’o
(Burundi) na Super Falcon ya Zanzibar.
Comments
Post a Comment