Meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe akimkabidhi jezi Makamu Mwenyekiti wa Simba Joseph Itang'are 'Kinesi' jezi katika hafla ya kuikabidhi timu hiyo vifaa itakavyotumia kwenye michuano ya kombe la Kagame.
Meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe akimkabidhi jezi Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako ikiwa ni sehemu ya vifaa walivyoiopatia kwa ajili ya michuano ya kombe la Kagame.Wanaoshuhudia ni Ofisa habari wa Yanga Baraka Kizuguto na Msaidizi wa Kavishe, Geoffrey Makau
PRESS
RELEASE
5/6/2013
Ikiwa ni sehemu ya
udhamini wake, bia ya Kilimanjaro Premium Lager imewapa vifaa vya michezo Simba
na Yanga kwa ajili ya michuano wa Kombe la Kagame iliyopangwa kufanyika kuanzia
tarehe 18 Juni mwezi huu.
Akikabidhi vifaa
hivyo Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe alisema, ‘‘
Bila ubishi Simba na Yanga ndio klabu kubwa za mpira Tanzania na zote zimefika katika fainali za mchuano wa Kombe la Kagame
kwa mara ya 19 sasa, haya ni mafanikio
makubwa kwa hizi timu, kama wadhamini wakuu wa timu hizi, Kilimanjaro Premium
Lager inaziunga mkono Simba na Yanga
katika harakati zao kucheza tena fainali za michuano hii ya kusisimua na ya
kihistoria.
Aliongeza kuwa Kombe la Kagame ni mashindano makubwa Africa
mashariki na kati, na ni jukwaa bora kwa wachezaji wetu kuonyesha vipaji
vyao dhidi ya wachezaji wa viwango vya
juu katika kanda hii lakini pia ni jukwaa zuri kwa wale wanaounda timu za taifa
kuchagua wachezaji.
“Ushirikiano huu baina
ya Bia ya Kilimanjaro na klabu hizi ni mizizi inayotokana na maadili katika
kazi, kufanya kazi kama timu na ile kiu ya
mafanikio. Na mafanikio ya ushirikiano
huu ni pamoja na kushuhudia mara kwa
mara timu hizi mbili zikitoa
wachezaji kwa timu ya Taifa (Taifa Stars) ambao wamekuwa na matokeo mazuri chini ya udhamini
wa Bia ya Kilimanjaro.
Tutaendelea kusaidia
timu hizi, na kuhakikisha tunapeleka mpira wa nchi hii kwenye kilele cha
mafanikio.
Meneja wa Bia ya
Kilimanjaro pia aliwataka Simba na Yanga
kuhakikisha wanaiwakilisha nchi yetu vizuri
katika mchuano huu mkubwa wa vilabu katika ukanda wa Afrika Mashariki na
Kati na kuwasihi kuchukua ushindi na
kurudi na kombe la 12 la Kagame kwa mashabiki wanaosubiria kwa hamu.
Comments
Post a Comment