SIMBA imeamua kuachana na beki Mganda Samuel Ssenkoom (pichani )baada
ya kutoridhishwa na kiwango chake tangu ajiunge na timu hiyo Juni 4 mwaka huu kwa ajili ya majaribio.
Habari za uhakika kutoka Simba ambazo Sports Lady Blog
imezipata zinaeleza kwamba,tayari uongozi umeshamkatia tiketi ya bus la tayari kumrejesha kwao nchini Uganda.
Kiongozi mmoja wa Simba amesema kwamba Senkoom
anatarajiwa kuondoka nchini wakati wowote kuanzia sasa baada ya kushindwa
kuonesha kiwango cha kuridhisha tangu atue nchini kwa majaribio.
Ssenkoon aliyeanza kujinoa na wenzake Juni 5 kupitia mazoezi yanayoendelea
kwenye uwanja wa Kinesi, ameshindwa kuonesha makali kama ilivyotarajiwa huku kocha mkuu wa Simba Abdallah ‘King’ Kibaden kwa
nyakati tofauti alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa haridhishwi na
kiwango cha Mganda huyo ambaye alikuwa nakipiga katika klabu ya URA.
Comments
Post a Comment