MUDY MATUMLA |
Akizungumza na mwandishi wetu mwandaaji wa mpambano huo Shabani Adios 'Mwaya mwaya' amesema mpambano huo utasindikizwa na mabondia mbalimbali wanaotamba katika masumbwi
Mabondia hawo ni Shafii Ramadhani atakayemenyana na Juma Fundi huku Swaleh Mkalekwa akipambana na Cosmas Kibuga
mpambano huo unaotarajiwa kuwa wa kukata na shoka wa raundi sita umekuwa wa kusisimua na kuzagaa katika vinywa vya mashabiki wa mchezo huo
Huku bondia Mohamed Matumla akimtahadhalisha mpinzani wake kuwa siku hiyo ato kuwa na msalia mtume kwani kawaida yake inajulikana Matumla mpaka sasa amepambana mapambano 13 akidroo matatu na kushinda 10 ata hivyo ame sisitiza kumuhangamiza mpinzani wake mapema kadri iwezekanavyo na kuwaomba wapenzi wa mchezo huo waje mapema kushudia anavyo mmaliza vinginevyo watakosa uhondo wa masumbwi Mbali na kuwepo na mpambano huo Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' atasambaza DVD za mafunzo ya mchezo wa masumbwi
CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika masumbwi
DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha kwa simu 0713406938 ili uweze kupata dvd hizo kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo
katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo ya mchezo
huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD
Comments
Post a Comment