Dar es Salaam, Tanzania, Juni 27, 2013: Tanzania Breweries Limited (TBL) chini ya
nembo yake ya Kilimanjaro
Premium Lager, inaendelea na
tamasha lingine kubwa la muziki lijulikanalo kama ‘Kili Music Tour
2013’ wikiendi hii mjini Tanga.
Tamasha hili
kubwa litafanyika Jumamosi ya
tarehe 29 Juni, 2013 mjini Tanga kwenye
kiwanja cya Mkwakwani na itajumuisha wasaniii 8 ambao ni Ally Kiba, Snura
Mushi, Professor J, Mwana FA, Recho, Mzee Yusuph, Roma na Kala Jeremiah.
Tamasha hili lililokuwa linajulikana kama KTMA Winners Tour
mwaka huu lilibadilishwa jina na kuwa Kili Music Tour ili kupanua uwigo wake
na kujumuisha wasanii walioshinda tuzo
za Kili Tanzania Music Awards, wasanii waliopendekezwa kwenye tuzo na wasanii
ambao hawakushiriki kwenye tuzo lakini ni vinara kwenye tasnia ya muziki
nchini.
Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager Bwana George
Kavishe alinukuliwa akisema “tumeona ni jinsi gani mkoa wa Dodoma uliitikia
wito na kushiriki kwa kikamilifu kwenye Kili Music Tour wikiendi iliyopita,
hivyo basi tunategemea Tanga itajumuika nasi ipasavyo kufanikisha tamasha
litakalofanyika mkoani hapo Jumamosi ya tarehe 29.”
Bwana Kavishe aliendelea kufafanua kuwa “mwaka huu ndani ya
staili ya “kikwetu kwetu” bia ya Kilimanjaro Premium Lager inahakikisha kuwa
kama kawaida inatoa bonge la kiburudisho kwa watanzania ikizingatia jinsi
watanzania tunavyojivunia mambo yetu ya kitofauti kama muziki wetu wa bongo
fleva, dansi yetu ya kiduku, kandanda letu lenye ushabiki wa simba na yanga,
lugha yetu ya kipekee na bia yetu ya Kilimanjaro iliyotengenezwa Tanzania, kwa
kutumia viungo vya kitanzania na watanzania.”
Msanii aliyebobea wa bongo flava ajulikanaye kama Professor
J (Joseph Haule) naye alisema “wakazi wa Tanga na vitongoji vyake wasubiri shoo
kubwa ya kufana kama waliyoipata wakazi wa Dodoma wiki iliyopita. Tunategemea
kuwashangaza wanatanga kwa kuwapa vionjo ambayo hawajawahi kuviona kwani mimi
na wasanii wenzangu tumejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa hatuwaangushi
mashabiki wetu na kuwa tutawapa bonge la kiburudisho!”
Comments
Post a Comment