Wachezaji wa Yanga wakisherehekea Ubingwa wa Ligi Kuu ya
Vodacom 2012/2013
Baada ya kuwa na mapumziko ya wiki mbili kwa wachezaji wake
na benchi la Ufundi, Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara
msimu wa 2012/2013 timu ya Young Africans Sports Club itaanza mazoezi wiki
ijayo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa 2013/2014.
Wachezaji wote na benchi la ufundi wataanza mazoezi siku ya
jumanne julai 02 saa 2 asubuhi katika uwanja wa shule ya Sekondari Loyola
kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom ambayo inatarajiwa kuanza agosti
24, 2013.
Kocha Mkuu Ernie Brandts ambaye yupo kwao nchini Uholanzi
kwa mapumziko ya wiki mbili, anatarajiwa kurejea siku ya jumatatu julai mosi
usiku kisha siku ya jumanne ataongoza mazoezi hayo kwa kushirikiana na kocha
msaidizi Fred Felix Minziro.
Yanga inaanza mazoezi mapema ili kujiweka katika mazingira
mazuri ya kuhakikisha inatetea ubingwa wake na kufanya vizuri katika mashindano
ya kimataifa, awali Yanga ilianza mazoezi june 3 kujianda na mashindano ya
kombe la Kagame ambalo serikali ilizizuia timu za Tanzania kushiriki mashindano
hayo kutokana na hofu ya usalama nchini Sudan..
CHANZO:www.youngafricans.co.tz
Comments
Post a Comment