Na Hosea Joseph
Mbali ya Kiemba, mchezaji Salum Abubakar ‘Sure boy’ wa Azam
FC alitwaa tuzo ya mchezaji bora chipukizi wa mwaka, huku Kocha wa Mtibwa Sugar
ya Turiani, Morogoro, Mecky Maxime akibeba tuzo ya Kocha Bora huku kipa bora
akiwa ni Hussein Sharif, pia wa Mtibwa.
Tuzo hiyo iliyofanyika kwa mara ya kwanza kwa lengo la
kuongeza ushindani kwa wachezaji kwenye klabu zao na timu za taifa, imefanyika
chini ya udhamini wa Kampuni ya Kishen Enterprises Ltd katika vigezo vya nyota
bora wa mwaka, chipukizi bora na kocha bora na kipa bora.
Kiemba aliibuka mshindi wa tuzo hiyo akiwabwaga Haruna
Niyonzima, Didier Kavumbagu wote wa Yanga, Kipre Tchetche (Azam FC) na
mshambuliaji Paul Nonga wa JKT Oljoro.
Kwa upande wa Sure boy, alitwaa tuzo yake akiwabwaga Hassan
Dilunga wa Ruvu Shooting, Idrisa Rashid wa Yanga, Frank Sekula na Shomari Kapombe wa Simba.
Mexime alijitwisha tuzo akiwashinda Charles Boniface Mkwasa wa Ruvu Shooting, Abdallah
Kibadeni wa Kagera Sugar na Jumanne Chale wa Tanzania Prisons. Sharif
aliwashinda kipa namba moja wa Simba na Stars, Juma Kaseja na Mwadin Ally wa
Azam FC.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Sputanza, Musa
Kisoki alisema washindi wa tuzo hizo wamepatikana baada ya uteuzi na upigwaji
kura uliofanywa na makocha na manahodha wa timu mbalimbali nchini.
Alisema vigezo vilivyotumiwa ni sifa ya mchezaji, nidhamu ya
ndani na nje ya uwanja, mafanikio yake kwenye klabu yake, uwezo wake binafsi na
mambo mengine yanayofanana na hayo na akawashukuru wote walioshiriki kwa namna
mbalimbali kufanikisha tuzo hiyo.
“Nawashukuru waliofanikisha tuzo hizi na wote mliofika kwani
huu ni mwazo, lakini naamini tutafikia mafanikio makubwa katika maandalizi
mengine badae yanayokuja kwa kuwa kila jambo huwa gumu mwanzoni,” alisema
Kisoki.
Alisema tuzo hizo zitakuwa zikitolewa kila mwaka chini ya
udhamini wa Toyo ili kuwaongezea wachezaji na makocha ari uwanjani wakati wa
mashindano mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.
Miongoni mwa viongozi walioshudhuria hafla hiyo ni Mama
Salma Kikwete aliyekabidhi zawadi za pikipiki na vyeti vya kuwakumbuka na
kuwapongeza wachezaji wakongwe wa zamani waliochezea timu ya taifa miaka ya
nyuma.
Naye mgeni rasmi katika tuzo hizo, Makamu wa Rais wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani aliwasihi Sputanza
kuwasaidia wachezaji katika vita ya dawa za kulevya na vitendo vya rushwa kwa
ajili ya kuhujumu timu.
“Nawapongeza wote kwa ujumla wenu kwa heshma hii mliyowapa
wachezaji kwani naamini itakuwa chachu katika kuendeleza mchezo wa soka
nchini,” alisema Nyamlani.
Comments
Post a Comment