MALKIA wa mipasho nchini pamoja na B Band inayoongozwa na
msanii Banana Zorro wanatarajiwa kutoa burudani katika shindano la kumsaka Redd's Miss Ukonga, linalotarajiwa kufanyika
Mei 25 mwaka huu katika Ukumbi wa Wenge Garden, Ukonga.
Mratibu wa shindano hilo, Rashid Kazumba alisema jana kwamba
maandalizi kwa ajili ya shindano hilo litakaloshirikisha warembo 17 yanaendelea
vema, huku washiriki wakiendelea kujifua.
“Maandalizi yote yameshakamilika kwa kiasi kikubwa ambapo
tunatarajia kuwa mashindano yatakuwa ya aina yake kwani warembo wana sifa na
tumedhamiria kumtoa Miss Tanzania kutoka katika Kitongoji chetu” alisema
Kazumba aliwataja
baadhi ya warembo watakaopanda jukwaani kuwa ni pamoja na Happyness Jackson,
Flosek Mwakanyamale, Glory Jigge, Annatolia Raphael, Musnat Hassan, Gift Swai,
Natasha Mohamed, Vanessa Magule, Queen John, Martha Gewe, Nancy Obasi,
Mwanamkasi Bakari na Diana Joachim.
Aidha, Kazumba aliwaomba mashabiki wa urembo wa jiji la Dar
es Salaam kujitokeza kwa wingi siku ya shindano hilo ambapo kiingilio kitakuwa
sh. 8000 kwa viti vya kawaida
wakati VIP watalipa sh.15,000.
Shindano hilo limedhamniniwa na kinywaji cha Redd's ambao ni washamini wakuu, Z.
Entertainment, Uefa Go City Pub, Mamushka Catering, Break Point, Saluti 5,
Times FM, Clouds FM, Business Times, Hiltec Resort pamoja na Kiota Jungle.
Comments
Post a Comment