AZAM FC KUREJEA NYUMBANI KESHO MCHANA


Timu ya Azam inatarajiwa kurejea nchini kesho (Mei 6 mwaka huu) saa 7 mchana kwa ndege ya Emirates kutoka Morocco ambapo jana (Mei 5 mwaka huu) ilicheza mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya AS FAR Rabat ya huko. 
Azam ilipoteza mechi hiyo kwa mabao 2-1, hivyo kutolewa katika raundi ya pili ya mashindano hayo. Mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es Salaam timu hizo zilitoka suluhu.

Comments