Daniel Nyalusi, Meneja wa tamasha la ZIFF
UONGOZI na Wandaaji wa Tamasha la Kimataifa la Filamu za
Nchi za Majahazi (Zanzibar International Film Festival (ZIFF) imesema kuwa
imebakisha siku moja pekee kwa wasanii wa Tanzania na wale wa Afrika Mashariki
kutuma kazi zao za filamu zitakazoingia kwenye
tuzo mbalimbali za tamasha hilo
linalotarajia kufanyika Juni 29 -Julai 7, mwaka huu.
Akizungumza leo Meneja wa Tamasha hilo,
Daniel Nyalusi alisema kuwa, toka ZIFF imeitisha upokeaji wa filamu kwa ajili
ya Tamasha hilo la 16 la Nchi za Jahazi mnamo Septemba 2012 na kuweka mwisho wa
kupokea Machi 31, 2013, hata hivyo kukawa na msukumo mdogo wa upokeaji wa
filamu toka Tanzania, tofauti na nje ambapo mpaka sasa wameshapokea filamu
zaidi ya 200 kwaajili ya uchaguzi wa jumla.
“Hii inasikitisha,
mpaka hatua ya mwisho wa zoezi la kupokea filamu za Kitanzania, ni
filamu 5 tu ndio tulizopokea, hivyo
kuamua kuongeza muda hadi Aprili 15, tunaomba wasanii wa Tanzania na wa Afrika
Mashariki kuchangamkia siku hizi mbili zilizobaki ilikutuma kazi zao” alisema
Nyalusi.
Pia Nyalusi alisema kuwa, katika tamasha hilo ambalo mwaka
huu linatimiza msimu wa 16, limesheheni mambo mbalimbali na kuwataka wadau
kulisubili kwa hamu.
Aidha, Nyalusi alieleza kuwa, kazi hizo za
Swahili Movie/Bongo Movie competition, ndizo filam zitakazotoa filamu
Bora ya Kitanzania, filamu Bora ya Afrika Mashariki na maeneo mengine (Categories).
Hata hivyo, Nyalusi alitumia wasaha huo kwa wasanii wote
kutuma kazi zao kwenye tovuti ya ziff ilikutuma kazi zao, ama katika ofisi zao
za ndani ya Ngome Kongwe Zanzibar.
Comments
Post a Comment