PAMOJA na kukubaliana na matokeo ya mechi ya jana dhidi ya
Azam, uongozi wa Simba unapenda kuweka rekodi wazi kwamba haukuridhishwa na
uchezeshaji wa mwamuzi, Oden Mbaga (pichani), hasahasa katika kipindi cha pili.
Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema kwamba, kwa bahati nzuri, msimamo huu wa Simba hauna hata chembe ya
ushabiki kwa vile hata washabiki waliokuwa katika upande wa watani wetu wa
jadi, nao pia walionekana kutofurahishwa na uchezeshaji wa Mbaga.
Mbaga ni mwamuzi mwenye beji ya Shirikisho la Soka Duniani
(FIFA) na katika hali ya kawaida ilitazamiwa mechi ingechezeshwa kwa viwango
vya kimataifa lakini hali ilikuwa kinyume chake.
Simba inaamini kwamba Mbaga hakuutendea haki mchezo ule wa
jana. Simba inasema hivi kwa sababu inataka mwamuzi huyo ajirekebishe na kwamba
matokeo ya mechi viwanjani yaamuliwe na ubora wa timu na si maamuzi yenye
utata.
Comments
Post a Comment