Michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inaendelea kesho
(Machi 2 mwaka huu) katika makundi yote matatu. Villa Squad itaivaa Ashanti
United kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam katika moja ya mechi za kundi B.
Kundi A ni mechi kati ya Kurugenzi ya Mafinga dhidi ya Mbeya
City wakati Polisi Iringa vs JKT Mlale, na Majimaji vs Mkamba Rangers
zilizokuwa zicheze kesho (Machi 2 mwaka huu), sasa zitaumana Machi 3 mwaka huu
mjini Iringa na mjini Songea.
Pia kundi B kesho (Machi 2 mwaka huu) ni Green Warriors vs
Transit Camp (Mlandizi) wakati keshokutwa (Machi 3 mwaka huu) Polisi Dar vs
Tessema (Karume) na Ndanda vs Moro United katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona
mjini Mtwara.
Mechi za kundi C kesho ni JKT Kanembwa vs Polisi Tabora
(Lake Tanganyika), Polisi Mara vs Polisi Dodoma (Karume, Musoma), Morani vs
Pamba (Kiteto) na Mwadui vs Rhino Rangers (Kambarage, Shinyanga).
Comments
Post a Comment