Semina elekezi kwa ajili ya michuano ya Copa Coca-Cola 2013
iliyokuwa ifanyike Jumanne (Machi 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam sasa
imesogezwa mbele hadi Machi 26 mwaka huu.
Uamuzi wa kusogeza mbele semina hiyo umetokana na maombi ya
wadhamini, Coca-Cola ambao katika tarehe ya awali watakuwa na shughuli nyingine
za kampuni hiyo.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaomba radhi
wajumbe kwa usumbufu wowote utakaokuwa umejitokeza kutokana na semina hiyo
kusogezwa mbele.
Hivyo, washiriki wa semina hiyo wanatakiwa kuripoti Dar es Salaam (TFF) siku
moja kabla (Machi 25 mwaka huu).
Washiriki hao ni makatibu wa vyama vya mpira wa miguu vya
mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar .
Pia waratibu wa mikoa wa mashindano ya Umoja wa Michezo wa Shule za Sekondari Tanzania
(UMISSETA).
Barua za mwaliko kwa ajili ya semina hiyo tayari zimetumwa
kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa.
Comments
Post a Comment