WAKATI baadhi ya uongozi wa Simba ukianza
kumeguka, kamati ya utendajhi ya klabu hiyo imeunda kamati ndogo ya ushindi ambayo itakuwa chini ya mwenyekiti
wake, Rahma Al Kharoos ‘Malkia wa nyuki’(pichani)
Ofisa
Habari wa Simba Ezekiel Kamwaga amesema leo kwamba kamati ya utendaji ya klabu hiyo
iliyokutana juzi, iliamu kuunda kamati hiyo kwa
kuzingatia kwamba bado ligi inaendelea na Simba ina mechi ngumu mbele ya
safari,kwa lengo la kusaidia timu kufanya vizuri katika mechi zake zilizosalia.
Alisema mbali na Malkia wa wajumbe waliopo
ndani ya kamati hiyo ni pamoja Sued Nkwabi, Joseph Itang’are Kinesi, Dan
Manembe na Francis Waya.
Alisema Kamati ya Utendaji ya Simba imeshtushwa na
kujiuzulu kwa Makamu Mwenyekiti,
Geoffrey Nyange na Zacharia Hans Poppe, ambapo tayari za kujiuzulu kwao zimefika
kwa Mwenyekiti na akiona maamuzi hayo yanafaa, ataamua kwa mujibu wa maslahi ya
klabu.
“Kamati ya Utendaji imeshtushwa na kujiuzulu
kwa wajumbe hao muhimu. Mchango wao ulikuwa bado unahitajika sana ndani ya
klabu. Michango yao ya hali na mali ndani ya klabu katika miaka mitatu
iliyopita ilikuwa chachu kubwa ya mafanikio yaliyopatikana,”alisema Kamwaga.
“Napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba wapenzi
na wanachana wa Simba kuwa watulivu katika kipindi hiki. Kamati yenu ya
utendaji iko imara na inataka kuwahakikishia washabiki kwamba hali si mbaya
kama inavyoonekana,”aliongeza Kamwaga.
Kamwaga aliongeza kwamba katika kipindi hiki
ambapo Makamu amejiuzulu na Mwenyekiti yupo nje ya nchi kwa matibabu, kamati
imeniteua Mzee Kinesi kuwa Kaimu Makamu Mwenyekiti hadi Mwenyekiti atakaporudi.
Katika ha tua nyingine, Kamati ya imeazimia kuanza
mchakato wa mazungumzo na kundi la Mpira Pesa ambapo lengo ni kuhakikisha
tunaondoa misuguano ya ndani kwa ndani baina yao kuweza kuunganisha nguvu na kuokoa timu
Comments
Post a Comment