KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Uganda,
Uganda Cranes, Bobby Williamson, ametangaza kikosi cha nyota 22
kitakachoikabili Liberia hapo Machi 24, wakiwemo nyota watatu wanaocheza timu
za Yanga, Simba na Azam.
Kwa mujibu wa kikosi hicho ambacho
kitaingia kambini Machi 17 kwa mechi hiyo ya kuwania tiketi ya kucheza fainali
za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil , nyota hao ni Hamis Kiiza wa
Yanga, kipa Abel Dhaira wa Simba na Brian Umonyi wa Azam.
Aidha, Williamson amemwita kiungo wa zamani
wa klabu ya Bunnamwaya, Boban Zirintusa anayekipiga katika klabu ya Power Dynamos ya Zimbwabwe na Kizito Luwagga
wa klabu ya Leixieos FC ya Ureno.
Wengine ni Denis Onyange wa klabu ya
Mamelodi Sundown na kipa Abel Dhaira
wa Simba ya Tanzania
na mshambuliaji wa Gor Mahia ya Kenya ,
Daniel Sserunkuma aliyeifungia Uganda
katika mechi ya kirafiki dhidi ya Rwanda , Februari mwaka huu.
Katika kikosi hicho, kocha Bobby amemwita
Patrick Ochan, aliyekosa mkwaju wa penalti katika mechi ya mwisho ya kuamua
timu ya kucheza fainali za Kombe la Afrika dhidi ya Zambia
na Martin Mutumba anayecheza soka nchini Sweden .
Timu hiyo itaanza mazoezi yake Machi 17
katika uwanja wa Taifa wa Mandela, mjini
Namboole.
Kikosi kamili
Makipa: Denis Onyango (Mamelodi Sundowns ya
Afrika Kusini), Dhaira (Simba ,
Tanzania ) na Hamza Muwonge (Vipers SC)
Mabeki: Denis Guma (SCVU), Simeon Masaba
(URA FC), Joseph Ochaya (Asante Koto, Ghana), Henry Kalungi (Railhawks, USA)
Isaac Isinde (St. George Ethiopia), Nicholas Wadada (Vipers), Godfrey Walusimbi
(CS Don Bosco, DRC), Andrew Mwesigwa (FC Ordabasy, Kazakhstan).
Viungo: Boban Zirintusa (Power Dynamos,
Zimbabwe), Kizito Luwagga (Leixieos, Portugal), Said Kyeyune (URA FC), Mike
Mutyaba (TP Mazembe, DRC) and Tony Mawejje (free agent), Musa Mudde (Simba SC),
Hassan Wasswa (KCC FC), Geoffrey ‘Baba’ Kizito (Sai Gon, Vietnam), Moses Oloya
(Vietnam)
Washambuliaji: Kiiza (Yanga, Tanzania),
Daniel Sserunkuma (Gor Mahia, Kenya), Geoffrey Massa (Yenicam, Cyprus), Brian
Umony (Azam, Tanzania), Emmanuel Okwi (Etoile Du Sahel, Tunisia)
Comments
Post a Comment