Maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wanatarajiwa
kushuhudia burudani ya kipekee kutoka kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya Fid Q na Da Stamina
katika tamasha Mahususi lililoandaliwa kwa ajili ya wakazi wa jiji la
Dar es Salaam siku ya jumapili ya pasaka.
Tamasha hilo litakalo fanyika
katika Fukwe za bahari ya Hindi maarufu kama (coco
Beach ) linatarajiwa kukonga nyoyo za
wakazi wa Dar es Salaam kwa kutuo burudani hiyo
bure kupitia tamasha lililoandaliwa na kampuni ya Vodacom Tanzania .
Akizungumzia Tamasha hilo Mkuu wa Kitengo cha udhamini na
Masoko wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa amesema kuwa lengo kuu ni kutoa
burudani kwa familia na wakazi wa Dar ambao wameendelea kuiunga kampuni hiyo
mkono na kuweza kuwaelimisha kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni
hiyo hivi sasa,kama vile Cheka Nao na Promosheni ya MAHELA inayomwezesha kila
mtanzania kushiriki na kujishindia fedha taslimu.
"Tumeandaa burudani hii Mahususi kwa wakazi wa Dar na
sehemu zake tukitambua fika kuwa katika msimu huu wa sikukuu familia nyingi
hukutana pamoja na kufurahi, hivyo tumeona ni wakati muafaka kutoa burudani kwa
wanafamilia,"
Twissa amesema kuwa kufuatia Ofa mpya ya Cheka Nao ambayo
inawawezesha wateja wa mtandao huo kupiga simu kwa gharama nafuu kwenda
mitandao mingine ambayo imeungwa mkono na Watanzania wengi wameona kuwa ni
vyema kuwapa shukurani kwa kuwaburudisha bure.
"Jambo la kipekee ni kuwa sasa wateja wa Vodacom
wanaweza kuwasiliana kwa gharama nafuu kwenda mitandao mingine kupitia
promosheni yetu ya Cheka Nao, sasa tumeona ni vyema Kucheka pamoja na wateja
wetu pale katika fukwe za Coco, alisema Twissa na kuongeza kuwa.
"Kutakuwa na burudani za aina nyingi pamoja na michezo
ya watoto hivyo wazazi wawalete watoto wao wakutane na watoto wenzao wacheze
pamoja, na pia burudani nyingine kama bembea
na michezo ya kuchora,"
Kwa upande wao wasanii watakao toa burudani katika tamasha hilo wamesema kuwa
wamejiandaa na kujipanga vyema kuwapagawisha mashabiki watakao jitokeza siku
hiyo na kutoa wito kwa wakazi wa dar es salaam kujitokeza kwa wingi siku hiyo.
Comments
Post a Comment