MSANII anayekuja kwa kasi
katika muziki wa bongo Fleva Amos Mwasanje ‘Ambulance’ amekamilisha kurekodi
video ya wimbo wake uitwao ‘Kakanyaga Matope’.
Ambulance amesema kazi ya kurekodi video hiyo iliyofanyika katika maeneo
tofauti ya jiji la Dar es Salaam imefanywa na mtayarishaji Fred K .
Alisema wimbo huo unatarajiwa kuwagusa wengi kutokana
na ujumbe ulipo ndani yake, hivyo amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula.
Hata hivyo, Ambulance amesema
hatoweza kuiachia hewani kwa siku za hivi karibuni kutokana na tatizo la
ving’amuzi ambalo kwa sasa ni kilio kwa watanzania wengi ambao wameshindwa
kumudu kuvinunua.
“Nawashukuru mashabiki wa
muziki wangu kwa kuendelea kuniunga mkono nawaahidi kuwatayarishia kazi nzuri
zaidi, hata hivyo kwa sasa siwezi kuiachia video hiyo mpaka mambo ya ving’amuzi
yatakapokaa sawa,’alisema
Kakanyaga Matope itakuwa ni
video ya nne kwa msanii huyo ambapo awali aliachia, Nifundshe Kukatika,Ukienda
nyumbani aliomshirikisha Tundaman na Mapepe Kinoma aliomshirikisha Ney wa
Mitego.
Comments
Post a Comment