SIKU
moja baada ya timu ya Simba kufungwa na Libolo ya Angola katika mechi ya kwanza
hatua
ya
awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, viongozi sasa wanatamani kumrejesha Mserbia
Milovan Cirkovik (pichani kulia).
Habari
zaidi zinasema hiyo haitokani na kufungwa bao 1-0 na Libolo tu, pia kushuka kwa
kiwango cha timu hiyo hivyo kuambulia sare katika mechi mbili za Ligi Kuu Bara.
Kwa
mujibu wa chanzo cha uhakika kutoka
ndani
ya uongozi wa klabu hiyo, tayari viongozi wameshamweleza Milovan kuhusu jambo
hilo,
lakini
ameweka ngumu akitaka kupewa chake kwanza.
Molovan
kwa sasa yupo nchini akifuatilia stahili
zake
zinazokadiriwa kufikia jumla ya dola 32, 000
za
Marekani; karibia sh mil 50 za Tannzania.
Milovan
aliyetupiwa virago baada ya kwisha kwa raundi ya kwanza Novemba mwaka jana, nafasi
yake ilizibwa na Mfaransa, Patrick Liewig.
Akizungumza jijini Dar es
Salaam jana, Milovan alikiri kuwa kwenye mazungumza na uongozi wa klabu hiyo
wakitaka arudi, lakini anataka alipwe kwanza haki zake kabla ya mambo mapya.
“Kweli uongozi umekuwa na
mazungumzo na
mimi ya kutaka kunirejesha
kuinoa Simba, lakini nimewaambia wanilipe kwanza fedha zangu kabla ya kuketi
kujadili hilo,” alisema.
Hata hivyo hakuna kiongozi wa
Simba aliyepatikana jana kuzungumzia suala hilo, huku Ofisa habari wa timu hiyo
Ezekiel Kamwaga simu yake iliita bila majibu.
Licha ya Simba kuwa chini ya jopo
la makocha wanne wakiongozwa na Liewig, imekuwa na mwendo wa kusuasua kiasi cha
mashabiki
kutaka kocha huyo arejeshwe.
Liewig amekuwa akisaidiwa na
Mzambia Moses Basena, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ na Idd Pazi kwa upande wa makipa.
Aidha, yupo Talib Hilal aliyetua
nchini kuongeza nguvu kwenye benchi la ufundi wakati timu hiyo ikijiandaa dhidi
ya Libolo ya Angola.
Katika Ligi Kuu, Simba inashika
nafasi ya tatu ikiwa na pointi 28, nyuma ya kinara Yanga yenye pointi 36 huku Azam
ikiwa ya pili kwa pointi 33.
Comments
Post a Comment