Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa
Tanzania Bara inaendelea kesho (Februari 27 mwaka huu) kwa mechi tano zitakazochezwa katika viwanja
tofauti.
Vinara wa ligi hiyo Yanga wataikaribisha Kagera Sugar kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
kwa viingilio vya sh. 5,000 (viti vya bluu na kijani), sh. 8,000 (viti vya
rangi ya chungwa), sh. 15,000 (VIP C na B) na sh. 20,000 (VIP A).
Mechi nyingine za ligi hiyo ni Coastal Union vs Ruvu
Shooting (Mkwakwani, Tanga), Polisi Morogoro vs Mgambo Shooting (Jamhuri,
Morogoro), JKT Ruvu vs Toto Africans (Azam Complex, Dar es Salaam ) na Mtibwa Sugar vs Tanzania
Prisons (Manungu, Morogoro).
Comments
Post a Comment