Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Yamo, Stanley Kevela
akizungumza na ujumbe wa Yanga Veterans (hawapo pichani) katika hafla ya
kuwakabidhi vifaa vya michezo jijini Dar es Salaam jana.
KAMPUNI ya Yono Action Mart ya jijini Dar es
Salaam imeipiga tafu ya jezi timu ya Yanga Veterans ambayo inatarajiwa
kushiriki Bonanza la wakongwe litakaloanza kutimua vumbi kwenye viwanja vya
Sigara, Chang’ombe kesho.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi jezi hizo
zenye thamani ya sh 600,000, Mwenyekiti wa Bodi, Yono Action Mart, Stanley
Kevela, alisema, wameamua kutoa jezi hizo kwa kuheshimu na kutambua mchango wa
nyota hao wa zamani katika klabu ya Yanga na Taifa kwa ujumla.
“Sisi Yono na Yanga ni marafiki na tuna bajeti
yetu kabisa kwa ajili ya kusaidia mambo mbalimbali tunayoombwa na Yanga, kwani
inapofanya vizuri inatufurahisha sana na hata kuimarisha ndoa zetu, maana
ikifanya vibaya hata wake zetu tunawachukia. Hivyo tunaiombea Simba izidi
kusuasua. Adui yako muombee njaa,” alisema Kevela na kuibua vicheko.
Kwa upande wake, nyota wa zamani wa yimu hiyo,
ambaye hivi sasa ni Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako, aliipongeza
kampuni ya Yono kwa ‘kupromoti’ michezo na si kwa Yanga tu, bali hata sehemu
nyingine, na kuzitaka kampuni nyingine kuiga mrfano huo.
Naye Katibu wa Yanga Veterans, Mwanamtwa
Kihwelo, kwa niaba yake, alishukuru msaada huo na kuwataka wadau wengine waige
mfano huo wa kuwekeza katika michezo, wakiunga juhudi za Rais Jakaya Kikwete,
kusaidia katika sekta hiyo.
“Tunamshukuru sana Yono, kwani amekuwa msaada
mkubwa sana kwetu, si kwa msaada huu tu, bali haya mipango yetu mbalimbali ya
kujikwamia kimaisha, ikiwamo uanzishaji wa Saccos,” alisema Kihwelo.
Naye beki mahiri, David Mwakalebela, alisema
msaada aliyowapa Yono ni dawa, kwani kushiriki michezo na kufanya mazoezi
kunaimarisha afya ya binadamu na kuepukana na maradhi mbalimbali.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na nyota wa zamani wa
Yanga, ambako ukiacha Mwalusako, Mwanamtwa na Mwakalebela, pia alikuwepo
Mohamed Hussein ‘Mmachinga’.
Bonanza hilo linaloshirikisha timu zilizokuwa
zikitamba enzi za Ligi Daraja la Kwanza. Mbali na Yanga ambayo itafungua pazia
na Pilsner, pia ziko Simba, Kariakoo Lindi, Coastal Union ya Tanga, Ushirika Moshi, Tukuyu Stars Mbeya, Pamba ya
Mwanza, Bandari ya Mtwara na Reli ya Morogoro.
Comments
Post a Comment