WACHEZAJI wa klabu ya Yanga
wamekuwa gumzo nchini Uturuki kutokana na kuonesha kiwango cha hali ya juu
katika mazoezi na michezo yake ya kujipima nguvu.
Yanga ambayo imepiga kambi ya
maandalizi nchini Uturuki imekuwa ikirteka mashabiki wa soka huko ambao hufika
kuishuhudia uwanjani.
Kwa mujibu wa mjumbe wa
kamati ya Utendaji ya Yanga, Abdallah Binkleb alisema baadhi ya wadau hao
wamevutika na viwango vya wachezaji wa timu hiyo kiasi cha kutaka kufahamu
zaidi taarifa zao.
“Kwa kweli kocha na viongozi
waliopo huko wanatuambia kuwa watu
wanawafuata sana kuomba kujua wasifu wa wachezaji kwani wanafurahishwa mno na
viwango vyao,”alisema.
Hata hivyo, Binkleb alisema
mpaka sasa hakuana wakala ama timu yoyote ya huko ambayo imeonesha nia ya
kutaka kumnunua mchezaji wa timu hiyo.
Yanga ambayo ipo huko
kujiandaa na michuano mbalimbali ikiwemo klabu bingwa Afria Mashariki na Kati ‘Kombe
la Kagame’ ambao ni mabingwa watetezi pamoja na mzunguko wa pili wa ligi kuu ya
Vodacom.
Yanga ikiwa huko imeshacheza
mechi mbili ikiwemo dhidi ya Arminia Biefeld ya Ujerumani na kutoka sare ya bao
1-1 kabla ya kutandikwa mabao 2-1 na Denizlispor Fc ya Uturuki mchezo uliopigwa katika dimba la Selen
Football-Kamelya Complex,nchini humo, jioni ya leo itashuka dimbani kukipiga na Emmen Fc inayoshiriki Ligi daraja la kwanza nchini Uholanzi.
Kikosi cha Yanga
kinachonolewa na kocha Ernie Brandts kimepiga kambi kwenye hoteli ya hoteli ya
Fame Residence Football ambapo pia wanafanya mazoezi.
Comments
Post a Comment