MABINGWA wa
ligi kuu ya Vodacom Simba Sc leo wameuanza vema mzunguko wa pili baada ya kuitandika African Lyon mabao 3-1
katika mchezo ulipigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Simba ambayo
ilikwenda nchini Oman kuweka kambi maalum ya kujiandaa na Ligi hiyo, iliutawala
mchezo huo jana zaidi sambamba na kutandaza kabumbu safi.
Ramadhan
Chombo ‘Redondo’ aliiandikia Simba bao la kwanza dakika ya pili akimalizia pasi
ya Mrisho Ngassa,kabla ya Ngassa kuandika la pili katika dakika ya 18 baada ya
kuwakimbiza mabeki huku akiwachambua na kumtungua kipa wa Lyon, Abdul Seif.
Katika
mchezo huo, Jacob Massawe wa Lyon alikosa bao akiwa yeye na kipa Kaseja katika
dakika ya 5, huku Ngassa naye akikosa mara mbili katika dakika ya saba na 14.Huku Massawe akikosa tena bao la wazi
katika dakika ya 17 baada kuwashughulisha
mabeki wa Simba na kukosa bao akiwa na kaseja.
Ngasa
aliipatia Simba bao la tatu katika dakika ya 36 akiwa ndani ya boksi dogo
akimalizia pasi ya Kiemba.
Wakati bao la kufutia machozi kwa Lyon lilifungwa katika dakika ya 60 mtokea benchi Bright Ike aliifungia
Lyon akimalizia pande la Fred Lewis.
MATOKEO MENGINE:
AZAM v KAGERA SUGAR 3-1
RUVU SHOOTING v JKT RUVU 1-0
JKT OLJORO v TOTO AFRICAN
POLISI MORO v MTIBWA SUGAR 1-0.
COASTAL UNION v MGAMBO SHOOTING 3-1
Comments
Post a Comment