Kikosi cha Simba
UONGOZI wa mabingwa wa
Ligi Kuu ya Vodacom, Simba Sc umepiga
hodi ubalozi wa Tanzania
nchini Angola
kwa ajili ya kusaka video za wapinzani wao kwenye ligi ya mabingwa Afrika.
Simba imbayo ilikuwa Oman
kwa kambi maalum ya maandalizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara utakoanza
Januari 26, pamoja na ligi ya mabingwa Afrika ambapo itaanza kwa kuivaa
Recretivo de Libolo ya Angola
kati ya Februari 17 na 19 jijini Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Simba alisema kwamba kocha mkuu wa timu
hiyo Patrick Liewig ametaka mikanda ya Video za mechi za wapinzani wao hao ili
kuweza kuifanyia kazi kabla ya kukwaana nao.
“Unajua wapinzani wetu hatuwafahamu vizuri hivyo tumeona ni
vizuri kusaka mikanda yao ili kuweza kuifanyia
kazi kabla ya kukutana nao na tayari tumeshauomba ubalozi wetu nchini Angola
utusaidie kwa hili,”alisema
Kuhusiana na kambi ya timu hiyo, alisema imekuwa na
mafanikio makubwa na kocha ameridhishwa na kiwango walichofikia wachezaji wake
baada ya kukaa pamoja kwa wiki mbili
sambamba na michezo mitatu ya kujipima nguvu na timu za huko.
“Kocha ameridhika na wachezaji kuanza kuelewani, hivyo
anaamini kwa kiasi kikubwa ametimiza malengo yake aliyojiwekea katika
kuhakikisha anaijenga timu tayari kwa mashindano yoyote,”alisema
Kaburu aliongeza kuwa, timu hiyo itafanya mazoezi ya mwisho
leo kabla ya kesho asubuhi kuondoka huko na itakapowasili nchini itaingia
kambini moja kwa moja kuendelea na maandalizi yake, kabla ya alhamis kuivaa
Black Leopards ya Afrika Kusini kwenye Uwan jaw a Taifa.
Ikiwa Oman Simba ilicheza mechi tatu za kujipima uwezo
ambapo ilianza kwa kukwaana na timu ya Vijana wenye umri chini ya miaka 23 na
kufungwa bao 1-0, kabla ya kufungwa 3-2 na Qaboos na juzi ikaitandika Ahili Sidabi mabao 2-1.
Comments
Post a Comment