Mbio za Kilimanjaro Marathon mwaka
huu zinatajiwa kuwa na washiriki wa kigeni wapatao 600 kutoka nchi zaidi ya 40.
John Addison, Mkurugenzi Mkuu
wa Wild Frontiers, waandaaji wa mbio hizo alisema katika taarifa yake kwa
vyombo vya habari jana kuwa mbio hizo zinaendelea kuwavutia washiriki wengi wa
kimataifa kutokana na jitihada za pamoja zinazofanywa na waandaaji pamoja na
bia ya Kilimanjaro Premium Lager katika kutangaza tukio hili. Hii ndi sababu
iliyochangia ukuaji wa mbio hizi pamoja na ushiriki kuongezeka kila mwaka.
Addison alisema washiriki wengi
zaidi watatoka Marekani ikifuatiwa na Uingereza. Nchi nyingine zinazotarajiwa
kushiriki ni pamoja na Canada, Japan, Uganda, Zimbabwe na Kenya. Nyingine ni
pamoja na Sweden, Australia, Hungary, Germany,
Zambia, Morocco, Swaziland, Nigeria na Malawi.
Zikiwa zimepangwa kufanyika Moshi
tarehe 3 Machi 2013, mbio za Kilimanjaro Marathon zitakuwa zimegawanyika katika
sehemu nne ambazo ni 42km Kilimanjaro Premium Lager Marathon, 21km Half Marathon, GAPCO Disabled Half
Marathon na Vodacom 5km Fun Run.
Mbio hizo pia zinatarajiwa
kuchangamshwa na ushiriki wa timu za makampuni ambapo wafanyakazi wa makampuni
wadhamini watashindana katika mbio ya nusu marathon kupitia shindano
litakalojulikana kama“Half Marathon Corporate Challenge”. Makampuni ambayo
yameishathibitisha kushiriki shindano hilo ni pamoja na TPC Sugar ambao ndio
mabingwa watetezi wa shindano hilo wakifuatiwa na CFAO Motors, TanzaniteOne na Tanga
Cement.
Addison alisema kuwa mbio za
Kilimanjaro Marathon zinaingia katika mwaka wa 11 tangu kuanzishwa zikiwa
zimesajiriwa rasmi na shikisho la riadha la kimataifa na kuongeza kuwa kutakuwepo
na vituo vya maji pamoja na viburudisho katika njia ya mashindano hayo.
“Mbio hii inafanyika chini ya Mlima
Kilimanjaro ambapo kila mtu anaweza kukimbia kwa raka kwani urefu wake kutoka
usawa wa bahari ni wastani wa mita 830 mpaka 1150 katika barabara nzuri yenye
lami. Inatarajiwa kuwa shamrashamra maana wananchi wengi watajitokeza pembezoni mwa barabara
kuwashangilia na kuwapa moyo wakimbiaji, na wakimbiaji wa kujifurahisha
wanaweza hata kusimama kupata kiburudisho njiani”, Addison aliitimisha.
Mbio hizo zinadhaminiwa na Kilimanjaro
Premium Lager (wadhamini wakuu), Vodacom Tanzania (5km Fun Run), GAPCO
(Disabled Half Marathon), Tanga Cement, CFAO Motors, KK Security, Keys Hotel,
TPC Sugar, TanzaniteOne, New Arusha Hotel na Kilimanjaro Water.
Comments
Post a Comment