WAKATI
klabu ya Simba ikiilaani Azam Fc kwa kumuuza mshambuliaji wao Mrisho Ngassa kwa
klabu ya El Mereikh ya Sudan ,
uongozi wa Simba umeishitaki Azam kwa Shirikisho la soka Tanzania (TFF).
Aidha Simbna imeiomba TFF kutotoa hati ya uhamisho wa kimtaifa ya Ngassa mpaka suala hilo litakapopatiwa ufumbuzi.
Azam Fc
juzi ilitangaza kumuuza Ngassa El Mereikh kwa dau la dola 75,000 huku pia ikitaraji kumlipa dola 50,000 kama
dau la kusaini mkataba wa miaka miwili.
Ofisa
habari wa Simba Ezekiel Kamwaga amesema kwamba, Azam wamefanya uhuni
katika kumuuza Ngassa kutokana na ukweli kwamba nyota huyo ana mkataba na Simba
ambao utamalizika Mei 31, 2013.
Alisema kuwa
makubaliano yaliyopo kwenye mkataba wa Ngassa ni kwamba,Simba na Azam zote zina
mamlaka na mchezaji huyo hivyo hakuna
timu yoyote itakayofanya maamuzi bila kuishirikisha nyenzake.
“Pia
mkumbuke pia pamoja na dau la dola 25, 000 tulilomchulia Azam Fc, Simba
iliingia gharama nyingine za kumshawishi zaidi kama
gari, donge nono n.k, pia tulimpa kazi maalum kocha wetu ya kuhakikisha
anapandisha kiwango chake,”alisema.
Comments
Post a Comment