Zamoyoni Mogela
Mohammed Mwameja
Mohammed Mwameja
KATIKA
kuhakikisha inafanya vema katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Bara na
michuano ya kimataifa, Simba imewarejesha nyota wake wa zamani wakiunda Kamati
ya Ufundi ya timu hiyo.
Nyota hao
waliojumuishwa katika kamati hiyo, chini ya mwenyekiti wake, Ibrahim Masoud
‘Maestro’, ni Zamoyoni Mogella, Madaraka Suleiman, Mohammed Mwameja na Boniface Pawasa.
Hivi
karibuni, Mwenyekiti wa Simba, Alhaj Ismail Aden Rage, alitangaza kuvunja
kamati zote kutokana na kushindwa kuleta ufanisi, ikimaliza raundi ya kwanza
ikiwa nafasi ya tatu nyuma ya Yanga na Azam FC.
Kamati
zilizovunjwa ni Fedha, Mashindano, Ufundi, Usajili na Nidhamu, ingawa tayari
alishamteua Zacharia Hanspoppe kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili.
Habari za
uhakika kutoka ndani ya Simba, zinasema Rage amewateua Mogella,
Mwameja na
Pawasa kutokana na uwezo na ushawishi kutokana na mchango wao kwa timu hiyo.
“Mwenyekiti
ameona aingize na nyota wetu wa zamani ambao kila mmoja alikuwa anawakubali,
hivyo kwa uwezo walionao kwa kiasi kikubwa watasaidia kwa namna moja ama nyingine
mafanikio ya Simba.
“Hawa
wamecheza ndani na nje ya nchi, pia wamekuwa karibu na soka hata baada ya
kuachana na mchezo huu…nadhani watasaidia sana kuleta mabadiliko katika kikosi
cha Simba,” kilisema chanzo kutoka ndani ya klabu hiyo.
Kiliongeza
kwamba, kamati hiyo itakuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na benchi la ufundi, huku
wachezaji wakianza mazoezi ya kujenga mwili ‘Gym’ wakimsubiri Kocha Mfaransa,
Patrick Lieweing.
Wajumbe
wengine kwenye kamati hiyo ni Joseph Itang’are ‘Kinesi’, Sued Nkwabi ambao pia
ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo na Said Tuliy.
Simba
inakabiliwa na mitihani miwili; Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo itaanzia
nyumbani dhidi ya CR Libolo ya Angola kati ya Februari 15 na 17, na kutetea
ubingwa wake wa Ligi Kuu.
Comments
Post a Comment