KILI STARS ILIPOREJEA VICHWA CHINI JANA


 Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars ‘ wakiwasili  jana katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam wakitokea nchini Uganda kushiriki michuano ya Cecafa Challenge iliyomalizika juzi. Kilimanjaro Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager. (Picha na Mpigapicha wetu).
 Wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars ‘ wakiwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam  jana mara baada ya kuwasili wakitokea nchini Uganda kushiriki michuano ya Cecafa Challenge iliyomalizika juzi. Kilimanjaro Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager. (Picha na Mpigapicha wetu).
 Wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars ‘ wakiwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam  jana mara baada ya kuwasili wakitokea nchini Uganda kushiriki michuano ya Cecafa Challenge iliyomalizika juzi. Kilimanjaro Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager. (Picha na Mpigapicha wetu).
 Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania bara ‘Kilimanjaro Stars’ Kim Poulsen akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana pamoja na timu wakitokea nchini Uganda kushiriki michuano ya Cecafa Challenge iliyomalizika juzi. Kilimanjaro Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager. (Picha na Mpigapicha wetu).
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars ‘ wakiwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam  jana mara baada ya kuwasili wakitokea nchini Uganda kushiriki michuano ya Cecafa Challenge iliyomalizika juzi. Kilimanjaro Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager. (Picha na Mpigapicha wetu).

Na mwandishi wetu
Timu ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars iliyoshiriki katika mashindano ya Cecafa Challenge yaliyomalizika Jijini Kampala Jumamosi, imerejea Jijini Dar es Salaam huku sasa ikitizamia kukutana na Chipolopolo ya Zamzbia Disemba 23.
Stars, ambayo inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, ilirejea jana jioni kwa ndege ya Precision Air.
Kikosi hicho chenye wachezaji 18, kilifanikiwa kutinga nafasi ya nne katika mashindano hayo baada ya kufungwa za Zanzibar Heros kwa penalty 6-5 na kutinga nafasi ya tatu.
Katika mashindano hayo, The Cranes ya Uganda ilifanikiwa kutetea taji na kubakiza kombe nyumbani. Hii nimara ya 13 kwa Uganda kutwaa taji hilo.
Akizungumza baada ya kurejea, Kocha Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen alisema mashindano haya yalikuwa muhimu sana kwa timu yake kwani vijana wamepata uzoefu baada ya kukutana na timu ngumu na zenye uzoefu.
“Mashindano yalikuwa mazuri…tulienda na nia ya kurudi na kombe lakini hatujafanya jivyo ila muhimu ni kwamba mashindano haya yametupa uzoefu mkubwa ili tuweze kujiandaa na mashindano mengine ambayo yako mbele yetu,” alisema.
“Tumefarajika kucheza na timu kubwa kama The Cranes ambayo ndio timu bora katika Ukanda wa Afrika ya Mashariki na Kati,” alisema.
Alisema sasa hivi macho ya wachezaji yote yako katika mchezo ujao wa kirafiki dhidi ya Chipolopolo ya Zambia kwani ni mechi ambayo itakuwa kipimo kikubwa kwa Stars kwa hivyo inahitaji maandalizi makubwa sana.
“Nawaomba watanzania wasikate tama kwa kuwa tunaijenga timu hawa ni vijana na ninaamini siku zijazo watafanya vizuri zaidi,” alisema Poulsen.
Kocha Kim Poulsen anatarajiwa kutangaza kikosi cha Stars kesho Jumatatu na amesema atawaita wachezaji wa Zanzibar pia ambao walicheza vizuri Kampala.
“Niliwaona wakicheza kwa hivyo bila shaka waliofanya vizuri watakuwemo kwenye kikosi hiki,” alisema.

Comments