mratibu wa onyesho la miaka 15 ya fm academia Nassib Mahinya na Nyoshi El Saadat
MASHABIKI wa muziki wa dansi
nchini ,wameombwa kujitokeza kwa wingi kwenye onyesho maalum la maadhimisho ya
miaka 15 ya bendi ya muziki wa dansi nchini Fm Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’
litakalofanyika kesho kwenye ukumbi Msasani Club.
Akizungumnza na waandishi wa
habari jana kwenye hoteli ya Southernsun jijini Dar es Salaam, Rais wa bendi
hiyo, Nyoshi El Sadat alisema wamejipanga vema kuhakikisha wanatoa burudani ya
uhakika.
Alisema kuwa kupitia onyesho
hilo, wanataka kuonyesha thamani waliytonayo mashabiki wa bendi hiyo na muziki
wa dansi kwa ujumla kupitia burudani ya nguvu.
“Litakuwa ni zaidi ya onyesho
kwani miaka 15 kwa bendi kuwa imesimama si kitu kidogo, lakini kikubwa ni kuwashukuru
mashabiki wetu kwa kutufanya tuwe juu tangu mwaka 1997 mpaka sasa,”alisema.
Nyoshi aliongeza kuwa, pamoja
na burudani ya aina yake ambayo itahusisha nyimbo zao kuanzia za albamu ya
kwanza, Hadija mpaka zile zilizopo kwenye albamu yao ya saba, pia wasanii waliowahi
kupitia bendi hiyo watapata kupanda jukwaani.
Naye mratibu wa onyesho hilo,
Nassib Mahinya kupoitia kampuni ya Sinai Entertainment alisema maandalizi
yamekamilika ambapo kiingilio kitakuwa sh 10, 000 kwa kila mmoja ambacho
kitamuwezesha kupata chupa moja ya bia ya Windhoek Lager.
Alisema mbali na FM Academia
pia kutakuwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wakiwemo Dogo Janja, PNC
na kundi la Mapacha Watatu.
Onyesho hilo limedhaminiwa na
Mabibo Beer Wine & Spirit, Mama Mbaga Catering, Africa Media Group, Chonapi
General Supplier, Benny Mlokozi Company , Big Solution, Mtanashati
Entertainment, Eliado Point View, Arafa Salon, Friendship Restaurant,
Saluti5.com, Tigo na Masters Club.
Comments
Post a Comment