Mkurugenzi wa Glitz Entertainment Dennis Busulwa 'Ssebo' akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na Toto Party maalum itakayofanyika Desemba 25 na 26 katika ufukwe wa Cine Club Mikocheni, kulia ni mratibu wa maendeleo ya biashara kanda ya Tanzania ya beki hiyo, Adewuvi Adekunle na kushoto ni mkuu wa masoko na bidhaa, Andrew Lyimo
KATIKA kusherehekea sikukuu ya Krismas, watoto kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es
Salaam wameandaliwa party maalum ‘Toto Party’ inayotarajiwa kufanyika Desemba
25 na 26 kwenye ufukwe wa Cine Club Mikocheni, jijini Dar es Salaam .
Alisema watoto watakaohudhuria tukio hilo watapata kushiriki michezo mbalimbali
ikiwemo soka, kuogelea, kuruka, huku pia wazazi wao nao watashindana katika
michezo mbalimbali ikiwemo kuvuta kamba.
Aliongeza kuwa katika siku hizo kutakuwa na fursa ya
ufunguaji wa akaunti maalum kwa watoto kutoka benki ya Eco Bank kupitia akaunti
maalum ya watoto iitwayo ‘Pambazuka’ ambapo kila mtoto atakayefungua akaunti
hiyo ataingizwa katika bahati nasibu maalum.
“Akaunti hii ni muhimu kwa watoto wote wenye umri chini ya
miaka 18 ambapo fedha zake ni mahususi kwa ajili ya kuwasaidia katika elimu,
hivyo tunaomba wazazi kujitokeza kwa wingi na pia kila anayehitaji kumfungulia
mtoto wake gharama ni sh 10,000,”alisema
Comments
Post a Comment