PAMOJA na
kutong’ara kwenye timu yake katika mzunguko wa kwanza wa ligi kuu ya Vodacom,
mshambuliaji wa Simba Abdallah Juma ameonekana lulu kwa timu nyingine baada ya
kuwaniwa na timu zaidi ya tano.
Nyota huyo
ambaye alisajiliwa na Simba mawaka jana akitokea kwa maafande wa JKT Ruvu,
aliweza kung’ara zaidi na timu hiyo kwenye mechi za kirafiki wakati wa
maandalizi wa ligi hiyo.
Habari
kutoka ndani ya uongozi wa Simba zinaekleza kwamba tayari vilabu vya Pamba ya
Mwanza, Coastal Union ya Tanga ,
Tanzania
Prisons ya Mbeya, African Lyon na Ruvu Shooting.
Kiongozi
mmoja wa Simba alisema hivi karibuni kwamba, timu hizo zimetuma maombi ya
kutaka kumsajili kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi hiyo pamoja na ligi
daraja la kwanza, lakini mpka sasa bado hawajaamua juu ya suala hilo .
“Ndiyo
hivyo bado hajuaamua juu ya suala la Abdallah kwanmi hata sisi pia ni mchezaji
muhimu kwetu…tunasubiri majadiliano ya kamati ya ufundi kwanza ndipo
tutakapotoa maamuzi na pia dau nono litazingatiwa,”alisema.
Aidha,
kiongozi huyo aliongeza kuwa nyota wao Haruna Shamte pia ameomba na klabu ya African
Lyon ambapo viongozi wa pande zote wapo
kwenye mazungumzo.
Comments
Post a Comment