Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom
ambao ni wadhamini wakuu wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara imepongeza
ushindi na kiwango kilichoonyeshwa na
Kilimanjaro Stars dhidi ya Timu ya taifa
ya Sudan jumapili iliyopita.
Katika mchezo wake wa kwanza wa fainali
za Cecafa zinazoshirikisha timu za taifa za nchi za Afrika Mashariki na Kati
zinazofanyika nchini Uganda ,
Stars imeanza vema kwa kupata ushindi wa mabao 2-0.
“Tunaipongeza Kilimanjaro Stars kwa
ushindi huo kwani ni ushindi unaotoa matumaini ya kuendeleza rekodi ya mara
kadhaa ya kufanya vema katika mashindano ya Cecafa.” Alisema Meza katika
taarifa yake ya pongezi kupitia vyombo vya habari.
Meza amesema kikosi bora cha timu ya
taifa ni taswira nzuri ya ubora wa soka la ndani ikiwemo ligi kuu ambayo
Vodacom imekuwa ikiidhamini na ambayo imeonesha kukua kiushindani na hivyo
kuzalisha wachezaji imara kwa mashindano ya kimataifa.
Stars ipo kundi moja na Somalia , Burundi
na Sudan na imeonyesha
kandanda safi na
la kuvutia na hatimaye kuvuna ushindi huo wa magoli mawili kupitia mshambuliaji
wake John Boko anayechezea timu ya Azam FC.
“Ni ushindi wa Watanzania wote na wadau
wanaoitakia mema soka ya Tanzania ,
kwetu Vodacom ushindi huu unatupa nguvu, ari na chachu zaidi katika dhamira
yetu ya dhati ya kukuza na kuendeleza mpira wa miguu nchini kwa faida ya
washabiki, vilabu, wachezaji na taifa kwa ujumla.”
Vodacom ndio mdhamini mkuu wa ligi kuu
soka Tanzania Bara kwa zaidi ya miaka sita na hivyo kuwa moja ya wachangiaji
wakuu wa maendeleo ya mpira wa miguu nchini mchezo unaangoza kwa kuwa na idadi
kubwa ya washabiki.
Comments
Post a Comment