TIKETI ZA KIELEKRONIKI ITAKUWA MUAROBAINI WA MAPATO-TFF


SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) linaamini kutumika kwa tiketi za kielektroniki katika mechi mbalimbali nchini utakuwa ni muarobaini wa tatizo la mapato. 
Benki ya CRDB ndiyo imepewa tenda ya kutayarisha tiketi hizo ambazo zitaanza kutunmika rasmi katika mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom mwezi Februari mwakani. 
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Rais wa TFF Leodger Tenga alisema kwamba hatua hiyo ni jambo la heri na muhimu sana katika kipindi hiki ambacho wadau wamekuwa wakilalamikia suala la upatikanaji wa mapato kiduchu. 
Alisema pamoja na uzuri wa jambo hilo, lakini wengi watashtuka na kutaka kurudisha nyuma mchakato huo utakaojenga heshima, lakini Shirikisho hilo halitakubali kurudishwa nyuma. 
“Najua wengi litawaathiri sana kwa namna moja ama nyingine na hivyo kuanza kuleta vikwazo ili lisifanikiwe, tumesimama imara kuhakikisha hili linatimia ili kujenga heshima,”alisema Tenga

Comments