SHIRIKISHO la soka Tanzania
(TFF) lipo katika mchakato wa kutaka kukutana na uongozi wa Shirikisho la soka
England (FA) ili kuweza kupata mwongozo wa jinsi ya kumpata nyota wa Tanzania
anayekipiga katika klabu ya Chelsea ya huko, Adam Nditi (pichani).
Katibu Mkuu wa TFFAngetile Osiah ameiambiaSports Lady leo kwamba lisema jana kwamba wamefikia
uamuzi huo baada ya awali kugonga mwamba ya kumpata mchezaji huyo kwa ajili ya
kumtumia katika timu ya taifa ya vijana.
Alisema alisema tayari
wameshawasiliana na mmoja ya maofisa ubalozi huo, Amos Msanjila ili aweze
kuwawekea maziungira mazuri ya kukutana
na FA kwa ajili ya kuzungumzia suala hilo.
“Mwanzo tulipogonga mwamba
kumpata mchezaji huyu mdipo tuliposhauriwa kuongea na ubalozi wetu ili wao
wazungumze kwanza na FA na kutuandalia mazingira ya kukutana nao na kuanza
mchakato wa kumuomba Nditi,”alisema
Osiah aliongeza kuwa anaamini
zoezi hilo litafanmikiwa na hivyo nyota huyo ataweza kuja kuyichezea timu ya
Taifa ‘Taifa Stars’ katika mechi za
kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia.
Comments
Post a Comment