BAADHI
ya wajumbe wa Kamati ya Usajili ya Klabu ya Simba, wanatarajiwa kwenda Kampala nchini Uganda kwa ajili ya kusaka nyota watakaowasajili
kwa ajili ya kuziba mapengo ya wachezaji wake watatu wa kimataifa waliowatema
hivi karibuni kutokana na kutoridhishwa na mchango wao dimbani.
Baada
ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara kumalizika, Simba imewatema Komambil
Keita wa Mali , Danniel
Akuffo wa Ghana na Pascal
Ochieng wa Kenya .
Mjumbe
mmoja wa Kamati hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina lake, alisema jana kwamba,
wanatarajia kuwapata wachezaji hao kupitia michuano ya Chalenji inayoendelea
nchini humo ikishirikishisha miamba 11 ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati,
pia Malawi
iliyoalikwa.
Alisema,
anaamini lengo lao litafanikiwa kutokana na ukweli kwamba, wachezaji wote
wazuri wanaotoka katika nchi hizo, ndiyo waliyomo kwenye vikosi vya timu zao za
Taifa zinazoshiriki michuano hiyo.
“Tumeona
baadhi yetu waende Uganda
kwenye Chalenji ili kusaka wachezaji watatu wa kimataifa watakaoziba pengo la
kina Keita, Ochieng na Akuffo, kwani huko kutakuwa na wachezaji wengi wazuri,”
alisema.
Kiongozi
huyo aliongeza kwamba, kwa upande wa wachezaji wa ndani, tayari wameishaanza
mazungumzo na baadhi ya nyota wanaotarajia kuwasajili katika dirisha dogo la
usajili linalotarajiwa kufungwa Desemba 15.
“Hatuwezi
kusema idadi kamili ya wachezaji wapya wa ndani tutakaowasajili, kwani mpaka
sasa kuna mjadala juu ya suala hilo ,
kuna wengine watapelekwa kwa mkopo, kuna wengine tutabadilishana na baadhi ya
timu,” aliongeza.
Kwa
sasa, Simba imebakiza wachezaji wawili tu wa kigeni, Mganda Emmanuel Okwi na
Mzambia Felix Sunzu.
Aidha,
Simba ipo katika mazungumzo na wachezaji kadhaa wakiwemo Mkenya Jerry Santo
anayekipiga Coastal Union ya Tanga, Juma Seif
‘Kijiko’ wa Yanga, huku pia ikiwa katika mpango wa kubadilishana wachezaji na
Azam Fc.
Comments
Post a Comment