SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) linatarajiwa
kuendesha kocha maalum kwa makocha wa leseni C na waandamizi inayotarajiwa
kuanza kesho hadi Desemba 10 katika Uwanja wa Amaan, Visiwani Zanzibar.
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ameiambia Sports Lady kwamba wameamua kuendesha kozi hiyo ili kuondoa dhana iliyojengeka ya kwamba
wamekuwa wakiwatenga Wazanzibar katika mambo mbalimbali.
Alisema kozi hiyo itaendeshwa na mkurugenzi wa
Ufundi wa Shirikisho hilo, Sunday Kayuni akishirikiana na mjumbe wa Shirikisho
la Soka Afrika (CAF), Ahmed Babekir kutoka Sudan.
Alisema baada ya kumalizika kocha kwa makocha wa
daraja hilo, itafuata ya makocha waandamizi itakayoanza Desemba 11 hadi 14
katika uwanja huo.
Alisema mara baada ya kufanyika kwa kozi hiyo
makocha waandamizi watafanyiwa tathimini na kupatiowa vyeti maalum vya daraja B
vinavyotambuliwa na CAF .
Comments
Post a Comment