MAONYESHO YA SARAKASI YA MAMA AFRICA YAFUNGULIWA DAR.


Trade Marketing Supervisor wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya TIGO Gaudens Mushi (kulia) akizungumzia maonyesho hayo ambapo amefafanua kuwa kuanzia tarehe 27 Septemba hadi Novemba 4 mwaka huu maonyesho ya sanaa ya sarakasi yatafanyika katika ukumbi wa Mancom Centre-New World Cinema Mwenge yakiambatana na programu ya nyimbo za kitamaduni na za kisiasa, upindaji wa viungo, michezo ya viini macho, michezo ya angani, michezo ya Piramidi, michezo ya Ufito na boriti.
Mkurugenzi Mkuu wa Mancom Entertainment Bw. Costantine Magavilla akizungumza na vyombo vya habari ambapo amesema maonyesho ya mwaka huu hayatakuwa tu bora bali pia yatakuwa ni maonyesho ambayo yanatukuza na kuunga mkono sanaa na utamaduni wa Tanzania.
Pichani ni Baadhi ya wanasanaa hao wakionyesha sanamu mfano wa mamba ikitembea wakati wa maandalizi ya maonyesho hayo.

Comments