TFF YAMLILIA MCHEZAJI WA ZAMANI WA SIMBA


Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Simba, Issa Kihange kilichotokea juzi (Julai 24 mwaka huu) jijini Dar es Salaam. 
Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti akiwa mchezaji Kihange alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezeaz ikiwemo Simba na CDA ya Dodoma, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima. 
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Kihange, klabu za Simba na CDA na na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. 
Mungu aiweke roho ya marehemu Kihange mahali pema peponi. Amina

Comments