KOZI YA GRASSROOTS YAFUNGULIWA


Kozi ya makocha wa mpango wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 imeanza leo (Julai 10 mwaka huu) kwenye ukumbi wa Msimbazi Center, Dar es Salaam. 
Wakufunzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ndiyo wanaoendesha kozi hiyo iliyofunguliwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah. 
Kozi hiyo itakayomalizika Julai 15 mwaka huu inashirikisha washiriki 35, na mwendelezo wa ile ya awali iliyofanyika Desemba 14-17 mwaka jana jijini Dar es Salaam. 
Gouinden Thandoo kutoka Mauritius ni mmoja wa wakufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wanaoendesha kozi hiyo.

Comments