SIMBA SC KWENDA MWANZA IJUMAA


KIKOSI cha mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba Sc kinatarajiwa kwenda jijini Mwanza ijumaa hii  kwa ajili ya kupeleka ubingwa wa ligi hiyo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema kwamba kikosi hicho  jumamosi kitacheza jijini Mwanza  na timu itakayotangazwa baadaye kabla ya jumapili kukwaana na Toto Africans katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. 
Baadhi ya wachezaji wa Simba walianza mazoezi ya uwanjani jana kwenye viwanja vya TCC Chang’ombe kwa ajili ya kujiandaa michuno ya Kagame inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi jijini Dar es Salaam juni 14.

Comments

  1. YANGA BOMBA-UHURU BRANCHJune 21, 2012 at 8:49 AM

    SIMBA MNAHANGAIKA NA HUU UBINGWA BALAA,HIVI NIWAULIZE KITI WANYAMA,KWANI MARA YA MWISHO KUCHUKUA UBINGWA HUU ILIKUA MWAKA GANI??MBONA KAMA MNAWEWESEKA SANA KAMA VILE HAMJALICHUKUA HILI KOMBE MIAKA ISHIRINI ILIYOPITA MAY BE,HEBU ACHENI ULIMBUKENI,JIANDAENI NA KAGAME AMBALO NI KOMBE LA KIMATAIFA ZAIDI NA AMBALO LIKO MITAA YA JANGWANI,ACHANENI NA KUTAPA TAPA NA KOMBE LA MBUZI AMBALO HATA TUKUYU STARS KUTOKA KIJIJINI TUKUYU IMEWAHI KULICHUKUA KIMYA KIMYA BILA KELELE KAMA HIZI ZENU


    SAYZ MDAU WA BOMBA,BOSTON,USA.

    ReplyDelete

Post a Comment