SAMATTA HUYOOOOO MAN CITY

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mbwana Samatta, huenda akajiunga na mabingwa wa Ligi Kuu England, Man City.
Habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam zinaeleza kwamba nyota huyo aliyeibukia Simba Sc kwa sasa yupo katika mazungumzo na mawakala wa Ulaya ili aweze kwenda kufanya majaribio Man City na hatimaye kujiunga nayo iwapo atafuzu majaribio yake.
Imeelezwa kuwa, mawakala hao wameshawasili Kinshasha, DRC na kuanza mazungumzo na uongozi wa klabu ya TP Mazembe kuhusina na nyota huyo ambaye pia anakipiga katika timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars.
Samatta alijuiunga na TP Mazembe akitokea Simba kwa dau la dola 200,000.

Comments

  1. Hii ndio mfano ya wachezaji wengine,,,ni hatua muhimu katika soka...

    ReplyDelete
  2. Dada acheni kuandika habari bila kufanya uchunguzi. Tuwekee umeipata wapi, siyo kuandika hearsay...Pili: Sheria za uhamiaji za Uingereza haitamruhusu Samata kucheza kwa hiyo siyo rahisi kwa Manichester City kumchukua huku wakijua kuwa hawezi kucheza...Tanzania haipo kwenye viwango vinavyokubalika kwenye sheria ya Uhamiaji...kwa hilo haliwezakani kabisa.

    ReplyDelete

Post a Comment